Saturday 26 April 2008

Wanaanza kuanguka, mmoja baada ya mwingine.

Alianza Edward Lowassa, akafuata Ibrahim Msabaha, na muda haukupita, Nazir Karamagi akaaachia ngazi.

Kwa kasi hii, tunaweza kufika mwaka 2010 ikawa hatuna kiongozi hata mmoja ambaye hajaguswa na Kiwanda cha Kashfa cha Tanzania (KKT).

Niliwahi kutabiri, bila kuwa na ushahidi madhubuti, kuwa itakapofika 2015 Tanzania itakuwa na nafasi ya kupata Rais safi, ambaye hana kashfa wala marafiki wenye kashfa, na ambaye hataogopa kuchukuwa hatua dhidi ya wale wenye tuhuma za kashfa.