Friday 31 October 2008

Nchi Inakwenda Kombo

Pamoja na kwamba Serikali inasema mambo yanakwenda vizuri, ukweli ni kuwa Serikali inaelemewa na matatizo ya kila aina.

Migomo ya walimu, ya wanafunzi, ya wafanyakazi. Kushindwa kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime, na hivi karibuni wastaafu wa Shrika la Bandari kuvua nguo barabarani wakishinikiza Serikali kulipwa mafao yao.

Serikali ikiendelea kujidanganya kuwa hakuna tatizo, itaendelea kupoteza majimbo ya uchaguzi kwenye Uchaguzi Mkuu 2010.

Wednesday 29 October 2008

Kimya Kikubwa Kina Mshindo

Nimekuwa kimya kwa muda, lakini nitaanza tena kuandika kwenye blog hii baada ya muda si mrefu.

Yako mengi ya kusema, lakini nitachagua yale muhimu katika kuchangia mawazo mbalimbali.