Sunday 9 November 2008

Serikali inatuangusha

Kuna habari zilitangazwa Mei 2008 kuwa Serikali ya Tanzania itachukuwa hatua za kisheria dhidi ya kampuni ya Norconsult kwa tuhuma kadhaa, ikiwa ni pamoja na kuendesha biashara bila kuandikishwa, na kukwepa kulipa kodi.
 
            Habari kamili :
            http://allafrica.com/stories/200805090429.html
 
Kuna msemo wa Waingereza: Closing the stable door after the horse has bolted. Una maana kitendo cha kuchukuwa hatua baada ya athari kutokea.
 
Norconsult imefanya kazi Tanzania bila kuandikishwa kwa miaka kumi bila bugudha. Inakisiwa kukwepa kodi zipatazo Sh.2.4 bilioni. Imeshinda kandarasi kusimamia miradi mikubwa ya ujenzi ikiwa ni pamoja na barabara ya Sengerema - Busagara (Sh.35.7 bilioni), na barabara ya Marangu - Rombo Mkuu (Sh.23.3 bilioni).
 
Haiingii kichwani kuwa kampuni imepata kazi kubwa kama hizo Serikalini na hamna mamlaka yoyote iligunduwa kuwa kuna walakini. Kwa miaka kumi!
 
Hapa kinachoonekana kutokea ni makundi yenye maslahi ya kisiasa na uchumi yameanza kupambana kwa kutoleana siri zao. Na hii inatokea sana kwenye mifumo ya siasa ambapo kundi moja likishinda uchaguzi hutokea kujaribu kuhodhi madaraka yote ya kisiasa, kiuchumi, na kijamii na kusababisha kundi lililonyimwa fursa linapoingia madarakani kulipiza kisasi.
 
Kuna msemo wa Kiswahili: Vita vya panzi ni furaha ya kunguru. Msemo unaofaa katika mazingira haya ni: Kunguru (wakubwa) wakigombana, panzi (raia) wanapata ahueni.

No comments: